Tuesday, March 18, 2008

Muungano nje ya Tip Top!



Katika hali ambayo naweza kuiita ya kushangaza...wale wasanii wawili maswahiba......Mb Dogg na mwenzake Deso, ambao sio siku nyingi zilizopita walijitoa kwenye kundi lao la zamani la...'Tip Top Connection' wameungana na kuunda umoja wao Chini ya jina la 'Wamanza Bay'.
Kwa mujibu wa wawili hao....lengo la muungano huo ni kusaidiana katika kazi zao za sanaa kama familia na wala sio kama kundi.

``Tumekuwa na mahusiano mazuri tangu tukiwa ndani ya kundi letu la zamani....tumeona iko haja ya kukaa pamoja na kushirikiana.....ni ushirikiano wa kupeana kampani katika mambo mengi ya kikazi,`` alisema Deso.

``Kila msanii anaweza kuendelea kufanya kazi zake kivyake na kutoa albam zake lakini, unafanya hivyo huku ukijua una mtu ama watu wa familia yako wanaokusapoti.....ndio maana nzima ya familia yetu hii,`` alisema Deso.

Hivi sasa kundi hilo linajiandaa kupiga picha za pamoja kwa ajili ya kuutangaza muunganiko wao...na wana imani mambo yakienda kama yalivyopangwa watafanya familia kubwa zaidi na kuibua vipaji vya wasanii wengi waliofichika.

No comments: